Maana na Maumbo ya Unyambulishaji wa Vitenzi katika Kigĩchũgũ

Unyambulishaji wa vitenzi ni mojawapo ya masuala yanayoshughulikiwa katika taaluma ya mofolojia katika lugha nyingi za Kiafrika. Makala hii inashughulikia unyambulishaji wa vitenzi katika Kigĩchũgũ, kwa kufafanua maana zinazowakilishwa na maumbo mbalimbali katika Kigĩchũgũ. Katika uainishaji wa Guthrie (1967), Kigĩchũgũ ni mojawapo ya lugha za Kiafrika ambayo hudhihirisha unyambulishaji. Nadharia ya Mofolojia Leksia (Kiparsky, 1982 na Katamba, 1993) na Kanuni ya Kioo (Baker, 1985) zimetumiwa kueleza maana za mofu nyambulishi katika vitenzi vya Kigĩchũgũ. Vitenzi vilivyotumiwa katika makala hii viliainishwa katika kauli sita za unyambulishaji na kujadili maana ambazo huwakilishwa na maumbo ambayo huundwa na mifanyiko ya unyambulishaji. Makala hii inachangia katika kuongeza maarifa ya kiutafiti kuhusu sarufi ya Kigĩchũgũ na kuhifadhi lugha ya Kigĩchũgũ katika maandishi kama mojawapo ya lugha za Kiafrika.
JIUNGE NASI ILI KUPOKEA MACHAPISHO KWENYE BARUA PEPE

Jarida hili hutokea mara moja kwa mwaka (Novemba) na huchapisha makala ambazo hazijawahi kuchapishwa katika taaluma ya Lugha, Isimu na Fasihi ya Kiswahili na lugha nyingine za Kiafrika. Makala yasiyozingatia masharti yaliyowekwa na wahariri hayawezi kuchapishwa.